Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP inahitajia msaada wa dharura wa dola milioni 44 kuhudumia walioathirika na ukame Kenya

WFP inahitajia msaada wa dharura wa dola milioni 44 kuhudumia walioathirika na ukame Kenya

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeripoti kuwa linahitajia kufadhiliwa, haraka iwezekanavyo, na wahisani wa kimataifa msaada wa dola milioni 44 ili kuhudumia operesheni zake nchini Kenya katika kiezi sita ijayo na kunusuru maisha ya umma ulioathirika na ukame. Ijapokuwa idadi ya watu wanaohitajia msaada wa chakula imeteremka kwa sasa, kutokana na mvua za karibuni, hata hivyo WFP bado itahitajia kupatiwa msaada wa kununua nafaka, chakula cha dharura ambacho hupendelewa zaidi na waathiriwa wa ukame.