Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wasomali wafurahia Kombe la Dunia, kinyume na 2010

Wasomali wafurahia Kombe la Dunia, kinyume na 2010

Nchini Somalia, vikosi vya kulinda amani vya AMISOM pamoja na serikali ya Somalia, zinajitahidi kulinda utulivu katika mitaa ya Mogadishu, usiku na mchana, ili watu waweze kufurahia kombe la dunia.

Wakati wa kombe la dunia lililochezwa Afrika Kusini, wanamgambo wa Al-Shabab walikatalia watu kuangalia mechi kwenye televisheni zao binafsi ama za migahawa. Sehemu nyingi zilifungwa. Mwaka huu hali ikoje? Basi Ungana na Priscilla Lecomte katika makala hii.