UM umetuma wataalamu watatu Cote d'Ivoire kudhibiti kemikali maututi
Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Kiutu (OCHA) imetuma timu ya maofisa wataalamu watatu katika Cote d’Ivoire kuisaidia serekali kudhibiti vyema tatizo liliozuka karibuni baada ya kugunduliwa taka za sumu ya kemikali zilizomwagwa mwezi uliopita katika mji mkuu wa Abidjan na kuhatarisha afya na usalama wa raia, kwa ujumla.~