Watoto milioni 4.5 Ghana watapatiwa matibabu dhidi ya minyoo
Wiki ijayo UNICEF, ikishirikiana na idara za ilimu na afya katika Ghana wanatarajiwa kujumuika kuanzisha huduma za siku nne zenye dhamira ya kuwapatia watoto milioni 4.5 waliopo katika skuli za serekali 28,000, matibabu dhidi ya maradhi ya minyoo.