Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vikosi vya Ethiopia vyawasili Darfur kujiunga na UNAMID

Vikosi vya Ethiopia vyawasili Darfur kujiunga na UNAMID

Kundi la awali la Batalioni ya Wanajeshi wa Miguu 114 wa kutoka Ethiopia wanaotarajiwa kujiunga na Vikosi Mseto vya UM/UA kwa Darfur (UNAMID) limewasili kwenye mji wa jimbo la Sudan magharibi wa El-Fasher Ijumamosi tarehe 16 Agosti 2008.