UM yaomboleza mauaji ya wafanyakazi wawili Usomali
Mark Bowden, Mratibu Mkazi wa Misaada ya Kiutu kwa Usomali amethibitisha hii leo, kutokea Nairobi, ya kwamba watumishi wawili wa UM waliuawa Ijumatano asubuhi kwenye mji wa Hargeisa, Usomali Kaskazini pale majengo ya Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) yaliposhambuliwa na watu waliojitolea mhanga, waliotumia gari liliokuwa na viripuzi.