Wanasesere wabeba historia ya wakimbizi kutoka Syria
Pakua
Mapigano nchini Syria yameingia mwaka wa saba sasa, nuru ya kumalizika ikiwa haionekani. Wananchi wamekimbilia nchi jirani kusaka hifadhi wengine wamesalia nchini humo, huduma za msingi za kiutu zikikumbwa na mkwamo. Kwa wale waliosaka hifadhi ikiwemo nchini Lebanon, wanasaka mbinu za kuelezea madhila yao na hata ndoto zao wakati huu ambapo milio ya risasi na makombora inalia kila uchao. Je wanafanya kitu gani ambacho pia kinawaingizia kipato ugenini huku wakisaidia wakimbizi wenzao? Ungana basi na Assumpta Massoi kwenye makala hii.