Mataifa yanapaswa kushikamana kusongesha agenda 2030 ya SDGs: Mweli
Pakua
Jukwaa la kisiasa la ngazi ya juu la Umoja wa Mataifa HLPF, kuhusu malengo ya maendeleo endelevu SDGs linaelekea ukingoni hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa likitarajiwa kukunja jamvi hapo kesho Julai 17. Wawakilishi mbalimbali kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wamekuwa hapa kwa takriban wiki mbili kujadili jinsi ya kusongesha malengo hayo endelevu. Miongoni mwao ni Gerald Geofrey Mweli, Katibu Mkuu kutoka wizara ya kilimo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amemweleza Flora Nducha wa idhaa hii kuhusu ushiriki wake katika jukwaa hili.
Audio Credit
Leah Mushi/Flora Nducha
Audio Duration
8'22"