Israel lazima ichunguze mauaji ya mwanamke wa kipalestina Ukingo wa magharibi:Mladinov
Mamlaka ya Israel imetolewa wito wa kuwawajibisha kisheria wale waliohusika na shambulio ambalo llimekatili maisha ya mwanamke mmoja wa Kipalestina na kumjeruhi mumewe katika Ukingo wa magharibi.
Wito huo umetolewa leo jumapili mjini Jerusalemkupitia taarifa ya mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu mchakato wa amani ya Mashariki ya Kati, Nickolay Mladenov, wakati akilaani vikali shambulio dhidi ya Aisha Al-Rabi, alieuawa Ijumaa kwa mawe ambayo yanadaiwa kurushwa na washambuliaji wa Israel. Mwanamke huyo ameacha watoto wanane.
Afisa huyo amesema anatambua kwamba uchuguzi umeshaanza na ameitaka serikali ya Israel kuhakikisha kwamba wahusika wanafikishwa mbele ya haki na kuwajibishwa. Ameongeza kuwamashambulio kama hayo hayana tija yoyote nayanaweza tu kulitumbukiza eneo hilo katika duru nyingine ya ghasia ambazo zitahujumu hatua za kuleta amani kati ya wa Palestina na Israeli.
Pia amemutolea wito kwa pande zote kulaani vitendo vya ghasia na kupinga ugaidi.
Hadi sasa hakuna tarifa zozote zilizotolewa kuhusu kilichipelekea mauaji hayo .