Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

maji

Watoto wakichota maji huko katika Ukanda wa Gaza
© UNICEF/Eyad El Baba

Hatimaye UNRWA yapokea mafuta

“Kufuatia ucheleweshaji wa wiki kadhaa, Mamlaka za Israel ziimeidhinisha nusu tu ya kiwango cha chini cha mahitaji ya kila siku ya mafuta kwa ajili ya shughuli za kibinadamu huko Gaza.” Amesema Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina UNRWA Philippe Lazzarini

© UNICEF

Mtoto 1 kati ya 3 anakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji - UNICEF

Mtoto mmoja kati ya Watoto watatu au saw ana watoto milioni 739 duniani kote - tayari wanaishi katika maeneo yaliyo na uhaba mkubwa au wa juu sana wa maji, na mabadiliko ya tabianchi yanatishia kufanya hali hii kuwa mbaya zaidi, imebainisha ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu kwa saa za New York, Marekani. 

Audio Duration
1'49"
Msichana mdogo nchini Zimbabwe anakunywa maji safi na salama kutoka kwenye kisima kilichorekebishwa kwa msaada wa Umoja wa Mataifa.
© UNICEF/Karin Schermbrucker

Ripoti: Mtoto 1 kati ya 3 anakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji - UNICEF

Mtoto mmoja kati ya Watoto watatu au sawa na watoto milioni 739 duniani kote - tayari wanaishi katika maeneo yaliyo na uhaba mkubwa au wa juu sana wa maji, na mabadiliko ya tabianchi yanatishia kufanya hali hii kuwa mbaya zaidi, imebainisha ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF iliyotolewa usiku wa kuamkia leo Jumatatu kwa saa za New York, Marekani.

Audio Duration
1'49"
© FAO/Seyllou Diallo

FAO inasisitiza kwamba maji ni uhai, maji ni chakula tusimwache yeyote nyuma katika hili

Leo ni siku ya chakula duniani na maadhimisho ya mwaka huu kwa mujibu wa shirika na chakula na kilimo FAO yanasherehekea moja ya rasilimali muhimu zaidi kwa maisha ya binadamu ambayo ni maji, kwani yanachukua asilimia 50 ya uso wa dunia, yanazalisha chakula na kuwezesha watu kuishi. 

Maudhui ya siku ya mwaka huu ni “Maji ni uhai, maji ni chakula, usimwache yeyote nyuma”.

Sauti
2'51"

23 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia wiki ya maji na kazi ya Umoja wa mataifa katika utoaji wa huduma za maji. Makala tunakuletea uchambuzi wa Ibara ya 8 ya Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na mashinani tunakupeleka jijini Mbeya nchini Tanzania, kulikoni? 

Sauti
9'57"
TANBAT 6/Kaptain Mwijage Inyoma

Walinda amani kutoka Tanzania TANBAT6 watoa huduma ya maji kwa wanakijiji nchini CAR

Tukiwa bado katika Wiki ya Maji ambayo imeanza tarehe 20 na itaendelea hadi kesho tarehe 24, TANBAT 6 ambacho ni Kikosi cha sita cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA), kwa kutumia magari wametoa msaada wa maji safi na salama kwa wanawake wa vijiji vinavyokabiliwa na uhaba wa maji mjini Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï. 

Sauti
2'5"
Wanakijiji cha Bisa  wakiwa tayari kupata huduma ya maji safi na salama baada ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania chini ya MINUSCA nchini Jamhuri ya Afrika ya kati kusambaza huduma hiyo kwa njia ya magari.
TANBAT 6/Kaptain Mwijage Inyoma

TANBAT6 watoa huduma ya maji kwa wanakijiji nchini CAR

Tukiwa bado katika Wiki ya Maji ambayo imeanza tarehe 20 na itaendelea hadi kesho tarehe 24, TANBAT 6 ambacho ni Kikosi cha sita cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA), kwa kutumia magari wametoa msaada wa maji safi na salama kwa wanawake wa vijiji vinavyokabiliwa na uhaba wa maji mjini Berberati mkoa wa Mambéré-Kadéï. Afisa Habari wa TANBAT 6 Kapteni Mwijage Inyoma na maelezo zaidi.

Sauti
2'5"

22 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Mapigano yanayoendelea huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC yakiendeshwa na vikundi vilivyojihami vya waasi yanaendelea kufurusha watu kutoka makwao, na hivyo wakimbizi hao wa ndani kushindwa kujikimu maisha yao ya kila siku. Malazi ni shida, makazi ni shida, halikadhalika chakula. Maisha yanakuwa ni changamoto kila uchao. Hali hiyo iko dhahiri kabisa jimboni Kivu Kaskazini ambako hata hivyo hatua za shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani, WFP kwa wakimbizi Oicha zimeleta ahueni.

Sauti
9'59"