12 Septemba 2018
Pakua
Hii leo jaridani Anold Kayanda anaanzia kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani ambako Baraza la Usalama limejadili jinsi ya kuimarisha ulinzi wa amani hususan usaizidi kwa nchi zinazochangia walinda amani. Ni kwa muktadha huo mkuu wa operesheni na mafunzo wa Jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ amezungumza na Idhaa hii kuona kile ambacho Tanzania inataka kuona kinafanyika. Kayanda anamulika pia jukwaa la kimataifa la kuchagiza biashara ya nje lililomalizika leo huko Zambia na kijana mmoja kaelezea imekuwaje amefanikiwa katiak biashara yake ya njugu na maembe ya kukausha. Makala ni kijana wa kike aliyetaka kujiua kulikoni? Na mashinani tunakwenda Kenya, riwaya na ukuzaji wa lugha ya Kiswahili. KARIBU
Audio Credit
Anold Kayanga
Audio Duration
12'18"