Uhuru wa vyombo vya habari wamulikwa hususan Afrika Mashariki
Pakua
Ulimwengu umeadhimisha mapema wiki hii siku ya uhuru wa vyombo vya habari, sherehe za siku hiyo kimataifa zikifanyika huko Jakarta, Indonesia, zikiratibiwa na shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO.
Katika ujumbe wake, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres alisema bado wanahabari wanakumbwa na vitisho, mashambulizi ya kingono, kujeruhiwa, kutiwa korokoroni na hata kuuawa.
Kwa mantiki hiyo, Bwana Guterres alisema huu ni wakati wa kila mtu kusimama kidete kutetea wana tasnia hiyo kwa lengo la kuepusha utoaji habari zisizo sahihi.