Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Shilingi moja ya leo ni shilingi mbili ya kesho: Kijana mfuga Sungura

Shilingi moja ya leo ni shilingi mbili ya kesho: Kijana mfuga Sungura

Pakua

Si kawaida sana kwa msomi barani Afrika kufanya kazi ya ufugaji tena kufuga sungura. Hii ni tofauti kwa kijana Peter Kagereki kutoka Kenya ambaye ni miongoni mwa washindi watatu watatu wa shindano la benki ya dunia kuhusu matumizi ya blogu kwa maendeleo, #Blog4Dev. Kagereki pamoja na mambo mengine anasema kauli ya mwalimu wake kuhusu uwekezaji akitumia mfano wa shilingi, imemwezesha kuwa mfugaji aliyejipatai kipato na kwa kutumia msaada wa teknolojia anasonga mbele.

Kwa undani zaidi sikiliza sehemu ya kwanza ya mahojiano yake na Grace Kaneiya.

Photo Credit
Peter Kagereki, kijana msomi kutoka Kenya ambaye sasa ufugaji wa Sungura umemletea nuru kwenye maisha na hata kumsafirisha hadi Washington D.C nchini Marekani kuzungumza na wakuu wa masuala ya fedha ulimwenguni. (Picha:Kwa hisani ya Benki ya Dunia).