Ni jukumu la kila mmoja katika jamii kuhakikisha SDGs na ajenda ya Afrika ya 2063 vinafikiwa: TZ
Pakua
Warsha ya siku mbili kuhusu masuala ya maendeleo endelevu yaani SDG’s na ajenda ya Afrika ya maendeleo yam waka 2063, imekamilika leo mjini Johanesburg Afrika ya Kusini.
Warsha hiyo iliandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa Maendeleo UNDP na serikali ya Kazakhstan.
Washiriki kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika yametuma wawakilishi kwenye warsha hiyo. Tanzania haikusalia nyuma iliwakilishwa na naibu katibu mkuu wizara ya fedha na mipango Amina Shaaban. Amezungumza na Flora Nducha wa
Idhaa hii na kuanza kumueleza Umuhimu wa warsha hiyo
(MAHOJIANO NA AMINA SHAABAN)