Mafunzo ya lugha huko DRC yabadili maisha ya vijana
Pakua
Wahenga walisema elimu haina mwisho na hivyo fursa yoyote ya kujifunza inapojitokeza ni vyema kuitumia ipasavyo kwani inaweza kubadili maisha siyo ya anayejifunza tu bali pia ya jamii yake. Mathalani huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo eneo la Fizi, vijana kupitia mafunzo ya lugha wameweza kunufaika na mpango wa mawasiliano kwa njia ya barua na wenzao walio ughaibuni. Je ni kwa vipi basi? Ungana na Langi Asumani, kutoka Radio washirika Radio Umoja iliyoko eneo la Fizi, jimbo la Kivu Kusini nchini DRC.