Samadi ya Ng'ombe yaboresha maisha ya mkulima Rwanda
Pakua
Shirika la umoja wa mataifa wa Maendeleo na Kilimo (IFAD) kwa kushirikiana na serikali ya Rwanda imeanzisha mfumo uitwao "FlexiBiogas" ambayo ni mbinu ya kunasa gesi ya methane kutoka kinyesi cha ng'ombe ili kujenga mtambo wa gesi safi. Kutumia biogas kama nishati ni njia mojawapot ya kupunguza matumizi ya kuni ambayo inazuia ukataji miti na mmomonyoko wa udongo. Je, ni jinsi gani maisha ya mwanakijiji huyu imeboreshwa?. Basi ungana na Amina Hassan kwenye makala hii.