Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la kigaidi nchini Urusi
![Muonekano wa mji wa Moscow, Urusi Muonekano wa mji wa Moscow, Urusi](https://global.unitednations.entermediadb.net/assets/mediadb/services/module/asset/downloads/preset/assets/2018/07/19-07-2018-NICA-471265-Moskva-River.jpg/image1024x768.jpg)
Muonekano wa mji wa Moscow, Urusi
Katibu Mkuu wa UN alaani shambulio la kigaidi nchini Urusi
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotekelezwa leo kwenye ukumbi wa tamasha nje ya mji wa Moscow, nchini Urusi ambapo takriban watu 40 wameripotiwa kuuawa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo jioni kwa saa za New York Marekani Katibu Mkuu Guterres ametuma salamu za rambirambi kwa familia zilizofiwa, wananchi pamoja na Serikali ya Urusi.
Pia amewatakia majeruhi wote ahueni ya haraka.