Uingereza yaahidi dola milioni 4 kwa WFP kusaidia waathirika wa ukame Madagascar

ILO/Marcel Crozet
Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP limeishukuru serikali ya Uingereza kwa mchango wa pauni milioni 3 sawa na dola za Kimarekani milioni 4.1 kwa shirika hili ili liwasaidie kwa chakula watu walioathirika na ukame katika majimbo ya Androy, Anosy na Atsimo Andrefana, Kusini mwa Madagascar.