Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Shirika la Amani Girls Home limetuepusha na ukatili wa kijinsia-Wanawake Mwanza, Tanzania 

Baadhi ya wanajamii waliosaidiwa na shirika la Amani Girls Home kupambana na umaskini mkoani Mwanza, Tanzania.
UN/Amani Girls Home
Baadhi ya wanajamii waliosaidiwa na shirika la Amani Girls Home kupambana na umaskini mkoani Mwanza, Tanzania.

Shirika la Amani Girls Home limetuepusha na ukatili wa kijinsia-Wanawake Mwanza, Tanzania 

Wanawake

Shirika la Amani girls home la Mwanza Tanzania limeanzisha mradi unaowawezesha wasichana hususani wale waliokumbwa na changamoto mbalimbali za kimaisha, ili waweze kufikia malengo yao kwa kuwapa ujuzi mbalimbali.  

Kupitia shirika hili lisilo la kiserikali, baadhi ya wanawake waliokuwa na changamoto za kimaisha, wamepewa ujuzi mbalimbali na sasa wanautumia kujikwamua hasa kiuchumi na hivyo kuepuka ukatili wa kijinsi ambao moja ya visababishi vyake ni utegemezi wa kiuchumi. 

Lucy Daudi ambaye ni mnufaika wa moja ya program za shirika la Amani Girls Home, akizungumza kwa niaba ya wengine, amesema shirika hilo limemkwamua yeye binafsi na wanawake wenzake.  

Saysarah Masalu Msimamizi Msaidizi Kitengo cha Familia na Maendeleo ya Jamii wa Amani Girls Home ameeleza kwa kina shughuli zao na mafanikio.  

Soundcloud