Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hatari kubwa yawakabili watoa huduma ya kutapisha vyoo-WHO

Julius Chisengo, (kushoto) na Selemani Juma (kushoto) wakiwa wamesimama mbel eya mtambo wao wa kunyonya majitaka baada ya kupakua choo kwenye eneo la Kigamboni-Umawa, jijini Dar es salaam nchini Tanzania mwezi Juni mwaka huu wa 2019.
WaterAid/ James Kiyimba
Julius Chisengo, (kushoto) na Selemani Juma (kushoto) wakiwa wamesimama mbel eya mtambo wao wa kunyonya majitaka baada ya kupakua choo kwenye eneo la Kigamboni-Umawa, jijini Dar es salaam nchini Tanzania mwezi Juni mwaka huu wa 2019.

Hatari kubwa yawakabili watoa huduma ya kutapisha vyoo-WHO

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Hatma ya wafanyakazi katika sekta za usafi  na hususani watoa huduma ya kutapisha vyoo kwenye nchi zinazoendelea ni suala linalostahili kushughulikiwa kwa dharura, umesema Umoja wa Mataifa, ukionya kuwa haki zao, afya na hadhi zao ziko hatarini.

Likiangazia hatari inayowakumba mamilioni  ya watu wanaosafisha vyoo au watapisha vyoo, mabomba na matenki ya maji taka, kabla ya kaudhimishwa siku ya choo duniani Jumanne  Novemba 19, shirika la afya duniani WHO linasema licha ya kuwa watu hao wanafanya kazi muhimu ya umma, afya zao ziko hatarini na wakati mwingi wao hutengwa.

Taarifa ya WHO iliyoambatana na ripoti mpya imesema wafanyakazi hao mara nyingi hukaribiana na uchafu wa kinyesi cha binadamu, na hufanya kazi bila ya vifaa au kinga kwa kutumia mikono yao, suala ambalo huwaweka kwenye hatari ya kuambukizwa magonjwa mengi.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa wanakata tu huduma hiyo muhimu inapofeli, wakati jamii inakumbana na kinyesi cha binadamu  kwenye mitaro, mitaani na kwenye mito au wakati vyombo vya habari vinaangazia kifo cha mfanyakazi wa usafi wa kutapisha vyoo ndipo hatma zao zinawekwa wazi.

Pichani ni Juma Hamis (kushoto) na Juma Ng'ombo, (kulia), hawa ni wafanyakazi wa majitaka wakiwa wameegemea kwenye bajaji yao waitumiayo kwenye kazi.
WaterAid/ James Kiyimba
Pichani ni Juma Hamis (kushoto) na Juma Ng'ombo, (kulia), hawa ni wafanyakazi wa majitaka wakiwa wameegemea kwenye bajaji yao waitumiayo kwenye kazi.

Juma Ng'ombo ni mfanyakazi wa majitaka kutoka Temeke, jijini Dar es salaam nchini Tanzania.

Mashirika ya kimataifa yakiwemo la Kazi duniani ILO, Benki ya Dunia na lile la Water Aid, yanataja sehemu tisa zilizofanyiwa  uchunguzi za wafanyakazi wa usafi kwenye nchi za kipato cha chini na cha wastani wanaotapisha vyoo na matanki ya maji taka na kukarabati mabomba ya maji taka.

Ripoti hiyo inasisitiza kuwa usalama wa usafi lazima uambatane moja kwa moja na mazingira bora kwa wale wanaofanya kazi ya kutunza huduma  za usafi na kulinda afya zetu, ikiongeza kuwa wafanyakazi  katika sekta ya usafi wamebaguliwa ikilinganishwa na wafanyakazi wa sekta zingine.

Kwa mujibu wa WHO, hali duni za usafi pekee husababisha hadi vifo 432,000 kila mwaka  vinavyotokana na kuendesha na pia huchangia kuenea  kwa magonjwa mengine .

Mtapisha choo huko Bangalore nchini India.
WaterAid/CS Sharada Prasad
Mtapisha choo huko Bangalore nchini India.