Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mangariba wadondosha nyembe na wakumbatia uhamasishaji dhidi ya ukeketaji

Mwanamke huyu zamani alikuwa ngariba, sasa amedondosha wembe na anashiriki katika ukeketaji mbadala kufuatia mafunzo kwenye kituo cha Masanga mkoani Mara. Kituo hiki kinapata msaada kutoka shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA. Maghariba pia wakidondosh
Warren Bright/UNFPA Tanzania
Mwanamke huyu zamani alikuwa ngariba, sasa amedondosha wembe na anashiriki katika ukeketaji mbadala kufuatia mafunzo kwenye kituo cha Masanga mkoani Mara. Kituo hiki kinapata msaada kutoka shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA. Maghariba pia wakidondosha nyembe wanakuwa na mradi mbadala wa kupata kipato.

Mangariba wadondosha nyembe na wakumbatia uhamasishaji dhidi ya ukeketaji

Haki za binadamu

Ili kufanikisha vita dhdi ya ukeketaji ni lazima washika dau wote washirikiane ili kuhakikisha kuwa tendo hilo la kikatili linaloendelezwa kwa madai ya utamaduni linatokomezwa.

Miongoni mwa wadau ni mangariba ambao iwapo watadondosha nyembe zao basi vita dhidi ya ukeketaji itakuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa.

Hali ni kama hiyo kwa mmoja wa mangariba akiwa mkoani Mara nchini Tanzania ambaye awali alikuwa analipwa shilingi Elfu 10 kwa kila mtoto anayemkeketa lakini kutokana na kampeni kutoka shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA, nchini  humo sasa anahamasisha jamii kuachana na ukeketaji kama alivyomwelezea Bright Warren wa UNFPA.

Ngariba huyo, bibi Bhoke amesema aliwakeketa mamia ya wasichana wakati akifanya kazi hiyo ambayo inakiuka haki za wasichana, hatahivyi kufuatia mwamko wa serikali na wadau ikiwemo UNFPA kutokomeza ukeketaji aliamua kuwachana na kazi hiyo ambayo kwa maneno yake ilikuwa inamletea kipato tosha.

Bibi Bhoke baada ya kuachana na vitendo hivyo vya kikatili alikata kauli ya kuhamasisha jamii ikiwemo mangariba wenzake kuachana na mila hiyo potofu kwani baada ya kupata elimu alielewa fika kuwa ilikuwa inaathari kwa wasichana waliokeketwa. Bibi Bhoke anasema mangariba wengine watatu wameamua kuweka visu chini na badala yake kujihusisha na kazi mbadala kwa ajili ya kujipatia kipato.