WHO yachapisha mwongozo wa tiba dhidi ya madhara yatokanayo na FGM

WHO inasema sambamba na mwongozo huo, kuna kijitabu cha kusaidia wahudumu wa afya na wakunga kushughulikia matatizo yatokanayo na FGM pamoja na madhara yake ikiwemo kutoka haja ndogo mfululizo na matatizo wakati kujifungua, na vyote vinapatikana kwenye wavuti wa shirika hilo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo, msemaji wa WHO, Tarik Jasarevic amesema FGM ni tatizo la dunia lakini limejikita zaidi Afrika, Mashariki ya Kati na Asia, likiwa limekumba zaidi ya wanawake na wasichana zaidi ya milioni 200.
“Ni muhimu sana wahudumu wa afya popote walipo waweze kutambua FGM na kuwatibu wanawke na wasichana kwa uhakika,” akiongeza kuwa ndio msingi wa kitabu hicho cha mwongozo wa utabibu na kingine ambacho kinasaidia kuwahudumia wanawake na watoto waliokumbwa na FGM sambamba.