Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Guterres akataa katakata serikali ya Guatemala kusitisha shughuli za CICIG

Askari akiwa katika doria katika jiji la Guatemala nchini Guatemala
World Bank/Jesus Alfonso
Askari akiwa katika doria katika jiji la Guatemala nchini Guatemala

Guterres akataa katakata serikali ya Guatemala kusitisha shughuli za CICIG

Haki za binadamu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Guatemala Sandra Jovel ambapo waziri huyo amemkabidhi Katibu Mkuu barua ya kumwarifu dhamira ya serikali ya Guatemala, kuvunja ya ndani ya saa 24 mkataba unaoanzisha kamisheni ya kimataifa dhidi ya ukatili nchini Guatemala CICIG.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu Guterres amekataa katakata kilichomo katika barua hiyo.

Badala yake amesema Umoja wa Mataifa umekuwa ukizungumza na serikali ya Guatemala kwa ngazi mbalimbali kwa kipindi cha miezi sita iliyopita kwa mujibu wa ibara ya 12 ya makubaliano ya kuunda CICIG ambapo mamlaka ya kamisheni hiyo yamepangwa kufikia ukomo tarehe 3 ya mwezi septemba mwaka huu wa 2019.

Kundi la wanawake waliuchora mchoro huu katika mji wa Guatemala ili kuunga mkono juhudi za UN Women dhidi ya ukatili dhidi ya wanawake nchini humo.
UN Women/Carlos Rivera
Kundi la wanawake waliuchora mchoro huu katika mji wa Guatemala ili kuunga mkono juhudi za UN Women dhidi ya ukatili dhidi ya wanawake nchini humo.

 

“Hadi kufikia tarehe hiyo, tunategemea serikali ya Guatemala kuendelea kutekeleza majukumu yake ya kisheria chini ya mkataba huo” Guterres amesema kupitia taarifa hiyo.

Katibu Mkuu anatarajia Serikali ya Guatemala kuzingatia shughuli zake za kimataifa ili kuhakikisha ulinzi kwa wafanyakazi wa CICIG, wote wa kimataifa na wa kitaifa.

Katibu Mkuu amekumbushia mchango muhimu wa CICIG katika kupambana na ukatili nchini Guatemala.