Chondechonde wapokeeni wahamiaji waliokwama melini Mediterranea UNHCR
Shirika la kuwahudumia wakimbizi duniani UNHCR limeziomba serikali husika kuwakubalia mamia ya watu ambao wamekwama katika bahari ya Mediterani wakiwa ndani ya meli ya the Aquarius kuingia nchini mwao.
Wito huo umetolewa jumatatu na mjumbe maalum wa UNHCR katika eneo la Mediterani ya kati,Vicent Cochetel, ikiwa leo ni siku ya pili tangu watu hao wakiwa baharini ndani ya meli baada ya kuokolewa jumammosi. |
Anasema watu hao wanakabiliwa na changamoto nyingi na wanahitaji msaada wa haraka kwani vitu walivyokuwa navyo kama chakula na maji vinapungua na suala la nani achukue dhamana na vipi mataifa yagawane jukumu hilo yatafuata baadae baada ya watu hawa kuondolewa kutoka majini. Italy mwaka huu 2018 imeshapokea takriban wahamiaji 13,706, hii ikiwa ni idadi ndogo ikilinganishwa na miaka iliyotangulia.
|