Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dunia tuliyonayo ni moja tu hakuna haja ya kuiharibu-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Waziri mkuu wa Sweden  Stefan Löfven, wakizungumza na waandishi wa habari bmjini Backåkra, Sweeden , wakati wa mwanzo wa ziara ya Katibu Mkuu na wajumbe wa baraza la usalama nchini humo.
Picha na Moa Haeggblom
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres na Waziri mkuu wa Sweden Stefan Löfven, wakizungumza na waandishi wa habari bmjini Backåkra, Sweeden , wakati wa mwanzo wa ziara ya Katibu Mkuu na wajumbe wa baraza la usalama nchini humo.

Dunia tuliyonayo ni moja tu hakuna haja ya kuiharibu-Guterres

Masuala ya UM

Sisi binadamu hatuna rukhsa  ya kuangamiza hii dunia moja tuliyo nayo, ama kukubali tofauti zetu kusababisa mateso na maumivu ambayo yanatuzuia kufaidika na manufaa ya ustaarabu.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akihutubia wandishi habari mjini Backara Sweden bada ya kuwasili ambako yeyé na wajumbe wa baraza la usalama watakuwa na kikao maalum  cha faragha  katika nyumba ya Katibu Mkuu wa zamani  wa Umoja wa Mataifa  Dag Hammarskjöld. Akisistiza kuhusu ustaarabu Guterres amesema


(SAUTI YA ANTONIO GUTERRES)
‘’Na ninaposhuhudia yanayoendelea leo , tunapoona migawanyiko mingi, tofauti za zamani zikirejea, migawanyiko mipya ikiongezeka mara dufu, migogoro ambayo inasababisha mateso makubwa duniani kote, na Syria ikiwa ndio mfano wa yote, ni muhimu kukumbuka maneno ya Dag Hammarskjöld.’’

Katibu Mkuu António Guterres na wajumbe 15 wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakiwa Backåkra, Sweden. Photo: Moa Haeggblom
Picha na Moa Haeggblom
Katibu Mkuu António Guterres na wajumbe 15 wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakiwa Backåkra, Sweden. Photo: Moa Haeggblom

Ameongeza kuwa Dag Hammarskjöld leo anabaki kama nembo madhubuti na mfano muhimu kwao kuweza kufanya mambo ambayo ni sawa, ilikuweza kuepuka utata na tofauti pamoja na kuelewa kwamba binadamu wote ni sharti kufanya kila liwezekanalo kuwa na dunia moja yenye utangamano.


Pia Katibu Mkuu pia amegusia Korea Kaskazini kuhusu uamuzi wake wa kusimamisha kwa muda majaribio yake ya nyuklia pamoja na urushaji wa  makombora ya masafa marefu akisema


(SAUTI YA GUTERRES)
“ Ninaimani Korea Kaskazini, mlango baado uko wazi wa nia ya amani wa kuondoa silaha za nyuklia kutoka rasi ya Korea.”


Pia amekariri azma ya uungwaji mkono wa mfumo wa Umoja wa Mataifa kutanzua mgogoro huo tena kwa njia za amani.