Guterres alaani shambulizi la kigaidi mjini Kabul:
Amani na Usalama
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali shambulio la Jumamosi kwenye hoteli ya Intercontinental mjini Kabul nchini Afghanistan.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali shambulio la Jumamosi kwenye hoteli ya Intercontinental mjini Kabul nchini Afghanista.
Kufuatia taarifa iliyotolewa na msemaji wake, Antonio Guterres ametuma salamu za rambirambi kwa familia za waliopoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo kundi la kigaidi la Taliban limedai kuhusika huku akiwatakia ahuweni ya haraka majeruhi.
Pia Katibu Mkuu ameelezea mshikamano wake na serikali na watu wa Afghanistan katika wakati huu mgumu. Watu wapatao watano wanadaiwa kuuawa na wengine 16 kujeruhiwa huku mamia wakiokolewa wakati wa shambulio hilo.