Viongozi kukutana kujadili shughuli za AMISOM nchini Somalia.
Marais sita kutoka mataiafa yanayochangia wanajeshi nchini Somalia chini ya kikosi cha AMISOM wanakutana mjini Kampala Uganda mwishoni mwa wiki hii kwa kikao cha dharura kuzungumzia jitihada zonazoendelea za kukabilina na kundi la wanamgambo wa al Shabaab.Mkutano huo ambao utaongozwa na rais wa Uganda Yoweri Museveni unajiri baada ya madai kutoka kwa utawala mpya nchini Somlia unaoishutumuKenya kwa kuingilia masuala yake ya ndani na kuweka vizuizi mjini Kismayo.
Uganda ina wanajeshi wengi zaidi nchini Somalia pia wakiwemo wanajeshi kutoka Burundi, Kenya Sierra Leone,Djibouti na Somalia. Maafisa wanaohusika na masuala ya kigeni nchini Uganda wanasema kuwa mkutano huo ambao ni wa kwanza wa aina yake unataandaliwa kwenye eneo la starehe la Munyonyo.