Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahiga alaani mauaji ya mwandishi wa habari mjini Mogadishu

Mahiga alaani mauaji ya mwandishi wa habari mjini Mogadishu

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, Balozi Augustine Mahiga, ameshtushwa na kuhuzunishwa na mauaji ya mwandishi wa habari, Rahma Abdulkadir aliyekuwa akifanya kazi na Redio ya Abduwaq.

Watu wasiojulikana wanaripotiwa kumshambulia Bi Abdulkadir kwa bastola na kumuua katika mtaa wa Yaqshid, mjini Mogadishu.

Bwana Mahiga amekilaani vikali kitendo hicho, akisema kuwa Somalia inaendelea kuwa mahali pa hatari zaidi kwa waandishi wa habari, na kwamba picha hiyo ya hatari inatakiwa kubadilika.