Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF na washirika wasaidia waathirika wa Kipindupindu Haiti

UNICEF na washirika wasaidia waathirika wa Kipindupindu Haiti

Haiti nchi iliyoko katika visiwa vya Karibia ni nchi ambayo imekumbwa na ugonjwa wa mlipuko wa kipindupindu .Hii inatokana na majanga mbalimbali ya kibinadamu kama vile matetemeko ya ardhi yaliyosababisha watu wengi kukosa makazi na hivyo kuishi katika mazingira hatarishi.

Mlipuko wa kipindupindu umechangiwa na mikusanyiko ya watu katika nyumba zisizo rasmi, yakiwemo mahema, huku pia sababu nyingine inayotajwa kuchangia ugonjwa huo unaodhoofisha na kuua haraka ni misongamano mikubwa ya nyumba na matumizi mabaya ya huduma za kijamii kama vile maji na hata vyakula.