Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha mshtaka mkuu wa ICC aanza ziara juma moja nchini Kenya

Mwendesha mshtaka mkuu wa ICC aanza ziara juma moja nchini Kenya

Mwendesha mashata mkuu kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensouda yuko nchini Kenya kwa ziara ya juma ambapo anatarajiwa kukutana na mafisa wa ngazi za juu serikalini akiwemo rais na Waziri mkuu.

Akihutubia waandishi wa habari mjini Nairobi hii leo , mwendesha mashtaka huyo amesema anataraji kukutana na mashirika ya umma pamoja na baadhi ya mashahidi kwenye kesi inayowakabili wakenya wanne kwenye mahakama ya ICC ambapo pia atatembelea sehemu kadha za nchi kukutana na waathiriwa wa machafuko yaliyoshuhudiwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007. Jason Nyakundi na taarifa kamili.

(SAUTI YA JASON NYAKUNDI)