Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uwindaji haramu wa tembo waongezeka-Ripoti

Uwindaji haramu wa tembo waongezeka-Ripoti

Ripoti moja iliyoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imefichua juu ya kuongezeka kwa vitendo vya uwindaji haramu wa wanyama aina ya tembo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo kiwango cha uwindaji huo harama kimeongezeka mara dufu ikilinganishwa na mwaka 1989, kulipotolewa takwimu juu ya mwenendo huo.

Ripoti inasema viumbe vingi vya namna hivyo vinakabiliwa na wakati mwingine na vingine viko kwenye tishio la kutoweka kabisa.

Kuongezeka kwa uwindaji haramu huo kumechangiwa pakubwa na magendo ya biashara ya meno ya tembo yanayosafirishwa katika mataifa kadhaa.