Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maafisa wawili wa zamani wa jeshi la Rwanda wahukumiwa kwenda jela maisha:ICTR

Maafisa wawili wa zamani wa jeshi la Rwanda wahukumiwa kwenda jela maisha:ICTR

Maafisa wawili waandamizi wa zamani katika jeshi la Rwanda leo wamehukumiwa na mahakama ya kimataifa inayosikiliza kesi za mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994.

Maafisa hao wa zamani wamekatiwa kifungo cha maisha jela kwa kushiriki makosa ya mauaji ya kimbari yaliyofanyika katika siku 100 nchini Rwanda mwaka 1994. Watu takribani laki 8 waliuawa wengi wakiwa ni Watutsi na Wahutu wa msimamo wa wastani. Danford Mpumilwa ni afisa wa ICTR anayehusika na masuala ya umma anafafanua kuhusu hukumu na watu hao.

(SAUTI YA DANFORD MPUMILWA)