Uruguay yachunguza madai kuhusu wanajeshi wake walio kwenye kikosi cha UM
Umoja wa Mataifa umethibitisha kuwa uchunguzi umeanzishwa kutokana na tukio linalowahusu walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka nchini Uruguay wanaohudumu nchini Haiti. Kikosi cha wanajeshi wa UM nchini Haiti MINUSTAH kinasema kuwa kinafahamu madai yanayowalenga walinda amani hao yanayochunguzwa na wizara ya ulinzi ya Uruguay. Eliane Nabaa ni msemaji wa MINUSTAH.
(SAUTI YA ELIANE NABAA)