Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Balozi mwema ya UNICEF azungumzia umuhimu wa elimu

Balozi mwema ya UNICEF azungumzia umuhimu wa elimu

Mwimbaji mashuhuri duniani na balozi mwema wa shirika la kuwahudumia watoto la Umoja wa Mataifa, Shakira amezungumzia umuhimu wa elimu alipokutana na wanafunzi wa kiyahudi na wa kipalestina wanaosoma pamoja kwenye shule moja mjini Jerusalem.

Akiongea alipotembelea taasisi ya Max Payne ambapo kila darasa lina walimu wawili wanaofunza lugha ya kiarabu na kiyahudi, Shakira alisema kuwa ameridhika kama watu wengine kuwa kuwekeza katika elimu ndiyo njia bora ya kuleta amani na utulivu duniani. Tangu ateuliwe kama balozi mwema wa UNICEF mwaka 2003 Shakira amekuwa kwenye mstari wa mbele kwenye programu ya shirika la UNICEF ya kusaidia watoto kujiunga na shule.