Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uzalishaji wa kasumba umepungua Afghanistan:UNODC

Uzalishaji wa kasumba umepungua Afghanistan:UNODC

Ripoti ya utafiti wa kilimo cha kasumba nchini Afghanistan imeonyesha kuwa uzalishaji wa zao hilo umepungua kwa kiasi kikubwa.

Kwa mujibu ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na uhalifu na madawa UNODC ikilinganishwa na mwaka 2009 uzalishaji wa kasumba umepungua kwa nusu mwaka huu 2010. Mkurugenzi wa mtendaji wa UNODC Yury Fedotov amesema hii ni habari njema lakini kusiwe na matumaini makubwa sana kwani soko linaweza kutengamaa kwa wakulima wa kasumba hivyo ni lazima kitengo chake kiendelee kuliangalia kwa karibu suala hilo.

(YURY FEDETOV)

Ripoti hiyo ya utafiti iliyotolewa leo inasema kilimo bado kinaendelea katika maeneo machache ya majimbo ya Kusini na magharibi mwa Afghanistan, maeneo ambayo yameghubikwa na wanamgambo na mitandao ya uhalifu. Ripoti inasema kilimo hicho kimepungua kutoka ekari 193,000 mwaka2007 hadi ekari 123,000 mwaka huu, na majimbo mawili makubwa kwa usalishaji ni Helmand na Kandahari.

Tani 3600 pekee ndio zilizopatikana mwaka huu ikiwa ni pungufu ya asilimia 48. Sababu kubwa imetajwa kuwa ni ugonjwa ulioathiri kilimo hicho Helmand na Kandahar, lakini pia kushuka kwa bei ya zao hilo kwenye soko la kimataifa jambo ambalo limewafanya wakulima wengi kufikiria kuliacha.