Hali Iran inamtia wahka Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu
Navi Pillay, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu amenakiliwa akieleza ya kuwa ameingiwa wahka juu ya ripoti alizipokea zenye kudai wenye madaraka Iran wanatumia nguvu mno kudhibiti vurugu liliozuka nchini kufuatia matokeo ya uchaguzi wa uraisi uliofanyika wiki moja iliopita.