Mpatanishi wa UM/UA kwa Darfur asisitiza mapigano mapya yakomeshwe halan
Kwenye taarifa rasmi iliotolewa mjini Khartoum, Sudan na Djibril Bassolé, Mpatanishi wa Pamoja wa UM/UA kuhusu mpango wa amani kwa Darfur, ilidhihirisha wasiwasi wake juu ya kurudiwa tena kwa mapigano katika eneo la kusini, hali ambayo, alionya, kama haijadhibitiwa mapema itadhoofisha zile juhudi za kurudisha utulivu na amani kieneo, kwa kulingana na Mapatano ya Kiutu ya 2004 ya Kusimamisha Mapigano katika Darfur.