OCHA inasema hali Goma ni ya kubadilika
Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) inasema hali katika Goma ni yenye kubadilika na haina uhakika, na UM itabidi usubiri zaidi mpaka pale utulivu utakaporejea kwa wao kuweza kuwapelekea posho ya chakula wahamiaji wa ndani 50,000 waliong’olewa makazi kwa sababu ya mapigano.~