Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM yasaidia kupiga vita maradhi yanayoua migomba Afrika Mashariki

UM yasaidia kupiga vita maradhi yanayoua migomba Afrika Mashariki

Mradi wa pamoja uliotekelezwa na Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) na serikali ya Uganda, umewasaidia wakulima 3 000 kupambana na ugonjwa uliohatarisha kuangamiza uzalishaji wa mavuno ya ndizi za kupikia, zao kuu kwa raia milioni 14 wa Uganda ambao hulitegemea kwa mapato na chakula.