Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakulima wa Bukini wanasaidiwa kujitegemea chakula na FAO

Wakulima wa Bukini wanasaidiwa kujitegemea chakula na FAO

Eneo la Bukini mashariki limekamilisha wiki hii mradi maalumu wa Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) wa kuotesha chakula nje ya majira ya kupanda mbegu, hususan mpunga, mradi uliochukua mwezi mmoja mfululizo kutekelezwa, uliokuwa na makusudio ya kuhakikisha kutapatikana mavuno ya kutosha kukidhi mahitaji ya umma katika siku zijazo, na kwa Bukini kujiepusha kuagizisha chakula kwa wingi kutoka nchi za kigeni, katika kipindi ambapo bei ya chakula imefumka katika soko za kimataifa na nchi masikini huwa zinashindwa kuzimudu bei hizo.