Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNAMID yajaribu kurudisha hali ya matumaini kwa IDPs wa Darfur

UNAMID yajaribu kurudisha hali ya matumaini kwa IDPs wa Darfur

Rodolphe Adada, Mjumbe Maalumu wa Pamoja wa UM/UA kwa Darfur ameamrisha kupeleka kwenye kambi ya Kalma ya wahamiaji wa ndani katika jimbo la Darfur Kusini, timu ya maofisa wa mapolisi, washauri wa kijeshi, wahudumia haki za kibinadamu na vile vile maofisa wanaohusika na masuala ya kiraia kufanya uchunguzi juu ya tukio liliojiri mapema wiki hii huko ambapo wahamiaji wa ndani (IDPs) 31 waliuawa baada ya mapambano na vikosi vya usalama vya Sudan.