Mtumishi wa UNHCR aliyetekwa nyara Usomali kuachiwa bila madhara
Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limeripoti kukaribisha ripoti za kuachiwa huru kwa mkuu wa tawi la ofisi yao katika Usomali ambaye alitekwa nyara mnamo tarehe 21 Juni (2008) karibu na nyumba yake mjini Mogadishu na kundi la watu wasiojulikana waliokuwa wamechukua silaha.