Bassole amewasili Darfur kuanza rasmi kazi
Mpatanishi Mkuu wa Pamoja wa UM-UA kwa Darfur, Djibril Bassole amewasili kuanza kazi rasmi katika El Fasher hii leo, mji mkuu wa Darfur Kaskazini na ambapo pia yalipo makao makuu ya UNAMID. Baadaye Bassole ataelekea Nyala na El Geneina, miji mikuu ya Darfur Kusini na Magharibi.~~