Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wajumbe wa Baraza la Usalama wamewasili Cote d'Ivoire kukamilisha ziara ya Afrika

Wajumbe wa Baraza la Usalama wamewasili Cote d'Ivoire kukamilisha ziara ya Afrika

Tume ya wajumbe wa Baraza la Usalama wanaozuru Afrika imewasili Cote d\'Ivoire Ijumapili, wakiwa kwenye hatua ya mwisho ya ziara yao baada ya kutembelea mataifa ya Djibouti, Sudan, Chad na JKK. Ijumatatu wajumbe wa tume ya Baraza la Usalama wamefanyisha mazungumzo mjini Abidjan na Mjumbe Maalumu wa KM kwa Cote d\'Ivoire, Chuo Young-Jin na maofisa wengine wa ngazi za juu wa UM wanaohusika na huduma za amani nchini humo.