Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Miripuko ya UKIMWI ifasiriwe kihadhi kuwa ni "baa ya ulimwengu", inasema IFRC

Miripuko ya UKIMWI ifasiriwe kihadhi kuwa ni "baa ya ulimwengu", inasema IFRC

Shirika la Kimataifa la Jumuiya za Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu (IFRC) kwenye "Ripoti ya Mwaka ya Maafa Duniani" ilipendekeza janga la UKIMWI ulimwenguni, hususan katika Kusini mwa Afrika, litambuliwe kwa uzito unaolingana sawa na majanga ya mafuriko na njaa. Ripoti ilisisitiza ya kwamba fasiri ya UM juu ya maafa inalingana kikamilifu na athari za maradhi ya UKIMWI duniani.