UM unaendelea na operesheni za dharura katika Myanmar
Mashirika kadha ya UM bado yanaendelea kuhudumia misaada ya kiutu kwa umma wa Myanmar ulioathirika na Kimbunga Nargis, tufani ambayo iligharikisha sehemu kadha za taifa hilo katika siku kumi zilizopita. Hivi sasa Shirika la Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeshakamilisha misafara ya kupeleka Myanmar tani za metriki 360 ziada za chakula zitakazosaidia kuwahudumia lishe bora waathiriwa 750,000 mnamo miezi 3 ijayo. ~~
Sikiliza habari kamili kwenye idhaa ya mtandao.