Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNHCR atazuru Yemen kuzingatia hifadhi imara kwa wahamiaji wa Usomali na Ethiopia

Mkuu wa UNHCR atazuru Yemen kuzingatia hifadhi imara kwa wahamiaji wa Usomali na Ethiopia

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) Ijumatano ataanza ziara ya siku tano nchini Yemen, kushauriana na Serikali pamoja na wahisani wa kimataifa juu ya taratibu za kuchukuliwa shirika za kuwapatia wahamiaji wa Usomali na Ethiopia waliopo Yemen hifadhi bora. Guterres anatazamiwa pia kuhudhuria Mkutano wa Kikanda wa siku mbili juu ya Hifadhi ya Wahamiaji na Udhibiti Bora wa Uhamiaji wa Kimataifa, hususan lile fungu la raia waliotokea Pembe ya Afrika, mkutano utakaofanyika Sana\'a, Yemen kuanzia tarehe 19 hadi 20 Mei.