Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR itachunguza hadhi ya sheria mpya Utaliana inayofananisha uhamiaji na jinai

UNHCR itachunguza hadhi ya sheria mpya Utaliana inayofananisha uhamiaji na jinai

Shirika la Wahamiaji la UNHCR limeripoti kuwa litafuatilia, kwa ukaribu na makini zaidi, maana hakika ya sheria mpya iliopitishwa Ijumatano kwenye Mji wa Naples na Baraza la Mawaziri Utaliana, inayothibitisha kitendo cha uhamiaji usio halali kuwa sawa na kosa la jinai na uhalifu, ambao utastahiki hukumu ya kifungo cha muda mrefu gerezani kwa mtuhumiwa. ~~Kwa mujibu wa sheria hii mpya watu ambao ombi lao la kupata hifadhi ya kisiasa limekataliwa watalazimika kuondoka Utaliana bila ya fursa ya kukata rufaa; na wale wanaotaka kuomba hifadhi, ambao mara nyingi huingia nchini kwa njia zisio rasmi, wao watashitakiwa kufabya kosa la jinai lenye hukumu ya kifungo cha angalau miaka minne.~~ ~