Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Aila zilizong'olewa makazi na mapigano Sudan zinapatiwa huduma za msingi na IOM

Aila zilizong'olewa makazi na mapigano Sudan zinapatiwa huduma za msingi na IOM

Msemaji wa Shirika la IOM, Jean Phillipe Chauzay, aliwaambia waandishi habari katika Makao ya Ofisi za UM-Geneva juu ya huduma zao zinavyotekelezwa kufarajia kidharura misaada ya kihali kwa makumi elfu ya watu waliokimbia mapigano makali yaliotukia siku za karibuni kwenye mji wa Abyei,Sudan, baina ya majeshi ya taifa ya Sudan (SAF) na kundi la SPLM. Mji wa Abyei ni eneo lenye utajiri mkubwa wa mafuta na ni miongoni mwa zile sehemu za Sudan zenye kujulikana rasmi kama maeneo ya mpito, ambayo yanasubiri kupatiwa usuluhishi wa nani mwenye haki ya mamlaka.