Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF na V-DAY wanashirikiana kufyeka udhalilishaji wa kijinsia katika JKK

UNICEF na V-DAY wanashirikiana kufyeka udhalilishaji wa kijinsia katika JKK

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) pamoja na shirika lisio la kiserikali Marekani, ambalo hujulikana kama Shirika la V-Day au Shirika la Siku ya Ushindi, wameanzisha rasmi mjini New Orleans, kampeni ya kukomesha milele karaha ya kunajisi kimabavu wanawake katika JKK. Kampeni hii imekusudiwa kuhakikisha wale watu wanaoendeleza jinai hiyo ovu dhidi ya utu, wanashikwa na kufikishwa mahakamani kukabili haki.